

Washiriki wa miss Tabata 2010 wakipozi kwa picha katika ukumbi wa Da` West Tabata kabla ya kufika kamati ya miss Tanzania ilioongozwa na Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga
........................................................................................................................................................................
Lundenga awavulia kofia Miss TabataMkurugenzi wa Miss Tanzania Hashim Lundenga juzi alivutiwa na maandalizi ya warembo wanaoshiriki kwenye shindano la Miss Tabata ambao limepangwa kufanyika Ijumaa katika Ukumbi wa Dar West Park , Tabata.
Lundenga alisema wengi wa warembo hao wanasifa ya kushinda taji la Vodacom Miss Tanzania iwapo watajiamini na kutofuata tabia mbaya zinazofanywa na baadhi ya warembo waliyowahi kushiriki kwenye mashindano hayo.
Lundenga alisema hayo wakati alipotembelea kambi ya warembo wanaoshiriki Miss Tabata Jumapili katika ukumbi wa Dar West Park ambapo alisema kamati yake ni safi lakini tabia chafu zinazofanywa na baadhi ya warembo waliyowahi kushinda mataji mbali mbali zinafanya kamati yake ionekane haifai.
“Sisi tunaka na nyinyi siku 30 tu ambazo ni chache mno kutufanya tujue tabia zenu. Warembo wengi huwa wanaficha tabia zao wanaposhiriki lakini baada ya kushinda huwa huonyesha tabia zao mbaya kwa jamii,” Lundenga aliwaambia warembo hao.
“Tumegundua kuwa warembo wengi huwa nanapakaziwa na huonewa lakini hawana tabia mbaya,” mkurugenzi huyo alisema.
Warembo watakaoshiriki kwenye shindano la Miss Tabata ambalo litafanyika Ijumaa katika ukumbi wa Dar West, Tabata ni Ritha Swai (19), Upendo Paul (18), Jesca Mariwa (19), Ummy Mohamed (22), Benardina Mwita (18), Maria Mpete (22) na Cythia Baro (22).
Wengine ni Happyness Paul (21), Happy Mushi (20), Neema Chaky (18), Consolata Lukosi (20), Rose Anthony (23), Light Mziray (20), Bellynda Mselewa (20), Harrieth Mulumba (20), Lilian Andrew (19), Selina Wangusu (21) na Doreen Deus (18).
Warembo hao watakutana na majaji kesho kwenye prejudgement. Zawadi za washindi zitatangazwa Alhamisi kwenye kikao cha pamoja na waandishi wa habari itakayofanyika kwenye ukumbi wa Savanna Lounge kwenye jengo la Benjamin Mkapa Towers .
Bendi ya African Stars “Twanga Pepeta” watatumbuiza kwenye shindano hilo ambalo taji lake linashikiliwa na Everlyne Gamasa.
Miss Tabata imedhaminiwa na Vodacom, Overmeer Wine, East Africa Radio, EATV, Chicken Hut, Savanna Lounge, PSI, Fabak Fashion, Dreditto Entertainment, Screen Masters, Benchmark Productions, USA-Dars General Supplies.
Warembo zaidi ya 10 watafuzu kushiriki kwenye mashindano ya kanda ya Ilala na baadaye Vodacom Miss Tanzania.
Shindano la Tabata ni moja ya vituo viwili vilivyobakizwa kwenye kanda ya Ilala baada ya vingine vitatu kufutwa na waandaaji wa taifa.
Miss Tabata namba mbili wa mwaka jana Julieth William ndiye Vodacom Miss Tanzania namba tatu kwa sasa.

Mwenyekiti wa Miss Tabata Fred Ogot (katikati) akiwa na mratibu wa miss Tabata Mr GOD (kushoto) wakijadili jambo kabla ya kuwasili kwa Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga

Mrembo Light Mziray na Ritha Swai

Miss Tabata mwaka 2009 Everlyne Gamassa akiongea na washiriki wa miss Tabata 2010

Washiriki wa miss Tabata 2010 wakimsikiliza Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga

Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga

Warembo wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania

Miss Tabata mwaka 2009 Everlyne Gamassa

Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga akisisitiza jambo kwa washiriki wa miss Tabata 2010 alipokuwa akiongea nao katika ukumbi wa Da` West

Mrembo Neema Chaky akimuuliza swali Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga alipowatembelea kambini kwa ukumbi wa Da ` West Tabata

Mrembo Upendo Paul akimuuliza swali Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga alipowatembelea kambini kwa ukumbi wa Da ` West Tabata

Benardina Mwita naye pia alipata fursa ya kuuliza swali kamti ya miss Tanzania

Harrieth Mulumba akiuliza swali kwa kamati ya miss Tanzania



Warembo wa miss Tabata 2010 wakisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga

Miss Tabata mwaka 2009 Everlyne Gamassa

Baadhi wa washiriki wa miss Tabata 2010

Mwenyekiti wa Miss Tabata Fred Ogot


Walimu wa washiriki wa miss Tabata 2010, Sweet Ney (kulia) na Stella

Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga akisisitiza jambo kwa washiriki wa miss Tabata 2010

Mwenyekiti wa Miss Tabata Fred Ogot akiongea na warembo wake katika ukumbi wa Da' West Tabata.

Miss Tabata mwaka 2009 Everlyne Gamassa( kulia) Sweet Ney pamoja na Stella


Mwenyekiti wa Miss Ilala Mr. Kalikumtima akiongea na warembo wa miss Tabata 2010




Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga (kushoto) akiongea na warembo

''Mkifanya mambo ya utovu wa nidhamu sisi ndio tunalaumiwa ....nawaomba sana mjiheshimu katika kila jambo ili msiichafue sifa ya kamati ya miss Tanzania kwani ina miiko yake na kanuni zinazo iendesha....."

Warembo wa miss Tabata wakisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa viongozi wa kamati ya miss Tabata iliyowatembelea Jana jioni katika ukumbi wa Da' West Tabata.